Sunday, November 13, 2016

SHEREHE YA KUWAKARIBISHA MWAKA WA KWANZA CASFETA TAYOMI CHUO KIKUU MZUMBE

Siku ya Jumamosi ya tarehe 12 Novemba 2016, Familia ya Casfeta Tayomi Chuo Kikuu Mzumbe tuliwakaribisha wapendwa wetu wa mwaka wa kwanza.

Hawa ni baadhi ya mwaka wa kwanza wengi mno ambao wameungana nasi katika Familia yetu ya Casfeta Tayomi Chuo Kikuu Mzumbe.

 Ilikuwa ni ibada nzuri sana iliyojaa uwepo na udhihirisho wa nguvu za Mungu


Dr Titus Tossy kama "MENTOR" wetu, aliwakaribisha mwaka wa kwanza na kuwahimiza sana juu ya umuhimu ya kujiandaa kiroho(SPIRITUALLY) na kimwili(ACADEMICALLY) katika mazingira mapya waliyopo na hatua waliyoifikia.


 Mwaka wa kwaza wakiwa makini kabisa kusikiliza masomo wanayopewa na Watumishi wa Mungu



Baba yetu mlezi Mchungaji Emmanuel Meshy alikuwa pamoja nasi na alitupatia Neno la Mungu lililobadilisha kabisa fikira zetu ili ziweze kuendana sawasawa na Neno la Mungu



Ibada ilifuatiwa na kulishwa keki kwa mwaka wa kwanza pamoja na wanacasfeta tayomi wenyeji ndani ya Chuo kikuu Mzumbe



 Mwenyekiti wa Casfeta Tayomi Chuo Kikuu Mzumbe, Ndg Michael George Kishiwa akiwa makini kabisa kukata keki kwa ustadi ili watu waweze kula


MC wa sherehe hii Ndg David Kunonga Mezza akiwa makini kabisa kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa na Mungu akitukuzwa kwa kila jambo



Tunamshukuru Mungu sana kwa kutusaidia kufanikisha sherehe hii ya kuwakaribisha ndugu zetu mwaka wa kwanza. Na Sifa na Utukufu wote zimrudie yeye maana pekee ndiye anastahili. Amen

Wednesday, October 26, 2016

KARIBUNI MWAKA WA KWANZA CHUONI MZUMBE - MOROGORO




Karibuni Mwaka Wa Kwanza Wote, Chuo Kikuu Mzumbe. Njoo Umwabudu Mungu pamoja nasi, Katika Hema Yetu ya Kukutania, Eneo: Kilimahewa, Jirani kabisa na Hope Hostel, na Kilimani Park-Kitimoto area.
Barikiwa mno kwa Kuchagua Fungu Jema.

Kwa mawasiliano zaidi, wasiliana na namba za simu zilizoorodheshwa kwenye tangazo hapo juu.

Thursday, April 7, 2016

HUDUMA YA MAHUSIANO - CHAKWALE GAIRO

MATUKIO MBALIMBALI YA HUDUMA YA MAHUSIANO ILIYOFANYWA NA WANACASFETA TAYOMI MZUMBE CHUO KIKUU - 10/03/2016

 Tulipata nafasi ya kuwasaidia na kusema nao juu ya Neno la Mungu pia.

 Tunamshukuru Mungu kwa alichotupa, nasi tulitoa kwa moyo wote

 Tulipata fursa ya kukaa nao chini na kuongea mambo mbalimbali

 Walengwa walikuwa ni wazee, na watu wasiojiweza

Mungu Akubariki kwa yeyote uliyehusika kufanikisha hii huduma ya Injili ya Chakwale.

MOTIVATIONAL SEMINAR 11/04/2016 - 14/04/2016


Uongozi wa Casfeta Tayomi unapenda kukukaribisha katika MOTIVATIONAL Seminar itakayoanza tarehe 11/04/2016 mpaka 14/04/2016. Mhubiri atakuwa ni Rev Richard Chidundo kutoka God's Kingdom Family Ministries, vile vile utapata nafasi ya KUMJUA ZAIDI MUNGU katika Semina hii, kama moja ya somo katika mpangilio wa masomo yatakayofundishwa.






MUNGU AKUBARIKI SANA


Monday, April 4, 2016

CHAKWALE OUTREACH MISSION - Day 5

MATUKIO MBALIMBALI YA SIKU YA TANO YA HUDUMA YA INJILI ILIYOFANYIKA CHAKWALE - GAIRO 10/03/2016


VOICE OF HEALING (VoH) wakimsifu Mungu






 Mwinjilisti Innocent Mapesa alihudumu siku hiyo

Umati uliofanikiwa kufika kwenye mkutano





 Wengi waliokoka na walifunguliwa kwa JINA LA YESU




Saturday, April 2, 2016

CHAKWALE OUTREACH MISSION - Day 4

MATUKIO YA CHAKWALE OUTREACH MISSION - Day 4               09/03/2016


 Waongofu wapya wakifundishwa NENO LA MUNGU na Mwalimu Shalom, namna ya kuishi kwenye wokovu


 VOICE OF HEALING Choir wakimsifu Mungu katika Roho na Kweli


 Praise Celebration ziliendelea katika viwanja vya mkutano


 Mwinjilisti Theopista Mutajwa alihudumu siku hiyo

Umati wa watu waliofanikiwa kufika kwenye mkutano







 Wengi walimpokea Yesu kuwa BWANA na Mwokozi wa maisha yao




Wote waliowekewa mikono walifunguliwa kwa JINA LA YESU




Eneo la maombi (ICU) iliendelea na kazi kama kawaida na wote waliofika eneo hili walifunguliwa hakika kwa JINA LA YESU


Thursday, March 31, 2016

CHAKWALE OUTREACH MISSION - Day 3

MATUKIO MBALIMBALI YA MKUTANO WA INJILI ULIOFANYWA NA WANACASFETA TAYOMI MZUMBE CHUO KIKUU, CHAKWALE - GAIRO 08/03/2016



Kikundi cha kusifu na kuabudu VOICE OF HEALING (VoH) cha Casfeta Tayomi Mzumbe chuo kikuu, wakimsifu Mungu.


 Praise Celebration zikiendelea.


 Mwinjilisti Alex Kiuko alihudumu siku hiyo


 Mwinjilisti Kelvin Ndonde naye alihudumu siku hiyo


 Baadhi ya watu waliofanikiwa kufika kwenye mkutano


 Wengi waliokoka na wote walifunguliwa kwa JINA LA YESU


 Watoto wa Chakwale waliombewa na wote walifunguliwa kwa JINA LA YESU

Eneo la kuombea wenye mapepo na wenye shida mbalimbali aka ICU, liliendelea na kazi kama kawaida